Friday, January 26, 2024

OMTO WAJA NA MAKUBWA 2024


Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule akizungumza wakati mkutano wa kwanza wa mwaka 2024 wenye lengo la  kukutanisha wanachama kufungua mwaka pamoja na kupanga mikakati mbalimbali ya kimaendeleo katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo. Miongoni mwa waadau walioalikwa katika mkutano huo ni Mfuko Wa Uwekezaji Wa Pamoja ulionzishwa na Serikali  (UTT Amis ), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) , Mstaafu Forum na wadau wengine wa Technolojia. Mkutano huo ulifanyika makao makuu mwa Taasisi hiyo Kitunda.

 

Mkurugenzi wa Mstaafu Forum, Charles Ligonja akitoa somo la ushirikiano kwenye vikundi wakati mkutano wa kwanza wa mwaka 2024 wenye lengo la  kukutanisha wanachama wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO),   kufungua mwaka pamoja na kupanga mikakati mbalimbali ya kimaendeleo katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo.

 

Ofisa Masoko wa Mfuko wa Uwekezaji wa Pamoja ( UTT Amis ), Medson Enock akitoa somo la uwekezaji wa hati fungani wakati mkutano wa kwanza wa mwaka 2024 wenye lengo la  kukutanisha wanachama Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO),  kufungua mwaka pamoja na kupanga mikakati mbalimbali ya kimaendeleo katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo.

 

Wadau Kutoka Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF)b wakitoa elimu ya kujiwekea akiba wakati mkutano wa kwanza wa mwaka 2024 wenye lengo la  kukutanisha wanachama wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO),   kufungua mwaka pamoja na kupanga mikakati mbalimbali ya kimaendeleo katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo.




Baadhi ya wanachama wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO),  wakisiliza mada zitolewazo wakati wa wakati mkutano wa kwanza wa mwaka 2024 wenye lengo la  kukutanisha wanachama kufungua mwaka pamoja na kupanga mikakati mbalimbali ya kimaendeleo katika taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo. Miongoni mwa waadau walioalikwa katika mkutano huo ni Mfuko Wa Uwekezaji Wa Pamoja ulionzishwa na Serikali  (UTT Amis ), Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) , Mstaafu Forum na wadau wengine wa Technolojia. Mkutano huo ulifanyika makao makuu mwa Taasisi hiyo Kitunda.

 

Saturday, November 25, 2023

JUKWAA LA WANAWAKE LALETA NEEMA KITUNDA

Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha akizungumza na wanawake wa Kata ya Kitunda jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo. Jukwaa hilo lilikuwepo hapo awali ila limefanyiwa uhuishwaji na wanawake wa kata hiyo.


Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Kitunda, Anna Haule (kulia) akizungumza wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo la kuwezesha wanawake kiuchumi ulifanyika jijini Dar es Salaam jana. Moja ya Lengo la Jukwaa hilo ni kuwa na sauti ya pamoja, kutafakari na kuibua miradi mbalimbali. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha, Diwani Viti Maalum, Eva Nyamoyo na Mwenyekiti wa UWT, Mwanaidi Makongo.]


Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha akikata keki kuashiria uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo.


Diwani Viti Maalum, Bi. Eva Nyamoyo akitoa somo la malezi ya watoto wakati wa uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo. Jukwaa hilo lilikuwepo hapo awali ila limefanyiwa uhuishwaji na wanawake wa kata hiyo.


Baadhi ya wanawake wa Kitunda wakihudhuria katika uzinduzi wa jukwaa hilo jijini jana.



Bibi Maendeleo Kata ya Kitunda, Betty Mzava akizungumza katika hafla hiyo.



Mtendaji Kata ya Kitunda, leticia Chipando, akitoa somo la usafi mahala pa kazi jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo.

Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha ( katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kitunda wakati baada ya kuzindua jukwaa hilo jijini Dar es Saaam jana.





                             

Saturday, November 18, 2023

WATEULE VICOBA WAKUTANA NA NEEMA YA OMTO

Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule akitoa elimu ya vicoba endelevu kwa wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho jijini Dar es Salaam jana. Mkurugenzi huyo alialikwa kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.


Mwalimu wa Wateule Vicoba, Glory Munisi akitoa elimu kuhusu elimu ya fedha wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho kilichopo Ulongoni jijini Dar es Salaam jana. Wateule Vicoba inajumla ya vikundi 7 chini ya ,Mkurugenzi huyo.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo, Neema Mchau akizungumza wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni kuhusu masuala ya kuthamini familia pamoja na kuimarisa ndoa wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho jijini Dar es Salaam jana.


Baadhi ya Wanachama wa Wateule Vicoba wakisikiliza kwa makini mada zinazotolewa katika maadhimisho hayo.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule (katikati), Katibu wa OMTO, Eliwaza Joseph na Mkurugenzi wa Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo, Neema Mchau wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza maadhimisho ya maika 12 ya Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni jijini Dar es Salaam jana. 

Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule ( wa tatu kulia waliokaa ) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali ya mtaa, walimu wa vicoba mbalimbali pamoja na wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni baada ya kumaliza hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho jijini Dar es Salaam jana. Mkurugenzi aliahidi kufanya mipango ya kuvisajili vikundi vyote 7 vilivyopo katika kikba hicho pamoja na kushirikiano nao ili kupata fursa zilizopo kwenye Vicoba endelevu kama CRDB Imbeju.

Thursday, July 27, 2023

CRDB YAWAPA MITAJI WANACHAMA WA OMTO KUPITIA IMBEJU


 Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule ( wa pili kushoto), Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB, Vanessa Ng`wigulu ( kushoto ), Mwenyekiti wa kikundi cha Kipaji Changu, Anastazia Mateo ( wa pili kulia ) na Katibu wa Wanawake wa OMTO, Kandida Makubi wakionyesha fomu za kujaza kuelekea kupata mitaji wezeshi ya wanawake wajasiriamali na vijana ( IMBEJU) wakati wa kikao cha ndani cha viongozi wa vikundi vilivyopo chini ya taasisi hiyo jijini Dar es Salaama leo. Watakaojaza fomu hizo watapata mitaji isiyokuwa na riba kuanzia shilingi laki 2 hadi milioni 5.


Ofisa Maendeleo Kata ya Kitunda, Betty Mzava akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa kikao cha ndani cha viongozi wa vikundi vilivyopo chini ya Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) chenye lengo la kupanga mikakati ya kujaza fomu kuelekea kupata mitaji wezeshi ya wanawake wajasiriamali na vijana ( IMBEJU) jijini Dar es Salaam leo. Watakaojaza fomu hizo watapata mitaji isiyokuwa na riba kuanzia shilingi laki 2 hadi milioni 5.


Meneja Mahusiano wa Benki ya CRDB, Vanessa Ng`wigulu akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa kikao cha ndani cha viongozi wa vikundi vilivyopo chini ya Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) chenye lengo la kupanga mikakati ya kujaza fomu kuelekea kupata mitaji wezeshi ya wanawake wajasiriamali na vijana ( IMBEJU) jijini Dar es Salaam leo. Watakaojaza fomu hizo watapata mitaji isiyokuwa na riba kuanzia shilingi laki 2 hadi milioni 5.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule akitambulisha baadhi ya walimu wa vikundi vilivyopo chini ya taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo wakati wa kikao cha ndani cha viongozi wa vikundi vilivyopo chini ya Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) chenye lengo la kupanga mikakati ya kujaza fomu kuelekea kupata mitaji wezeshi ya wanawake wajasiriamali na vijana ( IMBEJU) jijini Dar es Salaam leo. Watakaojaza fomu hizo watapata mitaji isiyokuwa na riba kuanzia shilingi laki 2 hadi milioni 5.


Katibu wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Eliwaza Joseph akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa kikao cha ndani cha viongozi wa vikundi vilivyopo chini ya Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) chenye lengo la kupanga mikakati ya kujaza fomu kuelekea kupata mitaji wezeshi ya wanawake wajasiriamali na vijana ( IMBEJU) jijini Dar es Salaam leo. Watakaojaza fomu hizo watapata mitaji isiyokuwa na riba kuanzia shilingi laki 2 hadi milioni 5.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule ( kushoto)  akimtambulisha Katibu wa Wanawake wa taasisi hiyo, Kandida Makubi wakati wa kikao hicho jijini Dar es Salaam leo


Mweka Hazina wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Eugenia Shayo akizungumza katika hafla hiyo.




Baadhi ya viongozi waalikwa wakizungumza katika hafla hiyo


Maofisa wa Benki ya CRDB wakiendelea na zoezi la kufungua akaunti za IMBEJU jijini Dar es Salaam leo kwa wanachama wa vikundi vilivyopo chini ya Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) .



Baadhi ya Viongozi wa vikundi vilivyopo chini ya Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) wakimsikiliza kwa makini Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Anna Haule jijini Dar es Salaam leo.

Saturday, July 8, 2023

BONANZA LA KIJANA JITAMBUE LALETA NEEMA KITUNDA

 

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gimero and Sons Limited na Mlezi wa Taasisi ya kutoa Elimu kwa vijana na watoto kutambua vipaji vyao ya Green Kids and Youth Foundation, Anita Gimero Waitara ( wa pili kushoto), Mkurugenzi wa Taasisi ya Green Kids and Youth Foundation, Vailet  Samson Mwazembe ( wa tatu kushoto ) wakikabidhi mbuzi kwa mshindi wa kwanza wa Bonanza la kijana jitambue wa timu ya Kitunda FC, Kapteni Joseph Kateti ( kulia) jijini Dar es Salaam jana.Wengine kutoka kushoto ni Msemaji wa Okoa Jamii Kupitia Saratani ( OJAKUTA), Hadija Kondo na Mwenyekiti wake, Anne Migila.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gimero and Sons Limited na Mlezi wa Taasisi ya kutoa Elimu kwa vijana na watoto kutambua vipaji vyao ya Green Kids and Youth Foundation, Anita Gimero Waitara akizungumza wakati wa Bonanza la kijana jitambue liliofanyika katika viwanja vya Kitunda jijini Dar es Salaama jana. Bonanza hilo limehusidha timu 6 zilizopo katika kata ya Kitunda ni mwendelezo wa Taasisi kuksanya vijana pamoja na kuwakomboa wajitambue kifikra na kuepuka wizi, ubakaji, utumiaji wa madwa ya kulevya, ushoga na kuwa na maono endelevu.

Mkurugenzi wa Taasisi ya kutoa Elimu kwa vijana na watoto kutambua vipaji vyao ya Green Kids and Youth Foundation,Vailet  Samson Mwazembe akizungumza wakati wa Bonanza la kijana jitambue liliofanyika katika viwanja vya Kitunda jijini Dar es Salaama jana. Bonanza hilo limehusidha timu 6 zilizopo katika kata ya Kitunda ni mwendelezo wa Taasisi kuksanya vijana pamoja na kuwakomboa wajitambue kifikra na kuepuka wizi, ubakaji, utumiaji wa madwa ya kulevya, ushoga na kuwa na maono endelevu.


Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gimero and Sons Limited , Anita Gimero Waitara ( aliyevaa nguo ya njano ) akikabidhi zawadi ya pesa taslimu shilingi laki moja kwa washindi wa kwanza wa bonanza la kijana jitambue, Kitunda Fc lililofanyika katika viwanja vya Kitunda jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gimero and Sons Limited , Anita Gimero Waitara akitoa zwadi kwa mfungaji bora wa Bonanza hilo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gimero and Sons Limited , Anita Gimero Waitara ( wa pili kushoto) akitoa zawadi ya mpira kwa mshindi wa tatu Bonanza la kijana jitambue wa Timu ya Santos Fc, Yusufu Ramadhani jijini Dar es Salaam jana.

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Gimero and Sons Limited , Anita Gimero Waitara  akitoa zawadi ya mipira miwili kwa mshindi wa pili Bonanza la kijana jitambue wa Timu ya Chembe Fc, Akida Mohamed jijini Dar es Salaam jana.



Baadhi ya Vijana wa kata ya Kitunda wakihudhuria kusikiliza semina ya kijana jitambue baada ya kumaliza bonanza hilo lililofanyika katika viwanja vya kitunda jijini Dar es Salaama jana.











Wednesday, June 7, 2023

WANACHAMA WA OMTO WANUFAIKA NA IMBEJU YA CRDB

 Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule ( katikati ), Diwani wa Kata ya Kitunda, Victor Vedasto ( kushoto ), Meneja wa CRDB Tawi la Ubungo, Hollo Buyamba ( wa pili kushoto) na Meneja Mradi wa CRDB Foundation, Baraka Kiyolo ( kulia) wakiserebuka wakati wa kongamano la wajasiriamali lililowezesha kupata mitaji wezeshi kwa ajili ya kinamama wajasiriamali kupitia programu ya Imbeju lililofanyika jijini Dar es Salaam leo.


Meneja wa CRDB Tawi la Ubungo, Hollo Buyamba  akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa kongamano la wajasiriamali lililoandaliwa na Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) ikishirikiana na benki hiyo kumwezesha mjasiriamali kupata mtaji  kupitia programu yake ya IMBEJU. 

Diwani wa Kata ya Kitunda, Victor Vedasto akizungumza jijini Dar es Salaam leo wakati wa kongamano la wajasiriamali lililoandaliwa na Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) ikishirikiana na Benki ya CRDB kumwezesha mjasiriamali kupata mtaji  kupitia programu yake ya IMBEJU.

Meneja Mradi wa CRDB Foundation, Baraka Kiyolo akitoa elimu ya programu ya IMBEJU inavyomwezesha majsiriamali kupata mtaji wa biashara kupitia Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO) wakati wa kongamano la wajasiriamali lililoandaliwa na Taasisi hiyo jijini Dar es Salaam leo.

 Kikundi cha Kipaji Changu kikitumbuiza wakati wa kongamano hilo.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule  ( kulia), Meneja wa CRDB Tawi la Ubungo, Hollo Buyamba ( wa pili kulia), Meneja Mradi wa CRDB Foundation, Baraka Kiyolo ( wa pili kushoto) na Diwani wa Kata ya Kitunda, Victor Vedasto wakiagana baada ya kumaliza kongamano.

Baadhi ya akina mama wajasiriamali wakihdhuria katika kongamano hilo.

Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa benki ya CRDB, Kata ya Kitunda na Wakurugenzi wa taasisi mbalimbali katika makao makuu ya Taasisi hiyo yaliyopo Kitunda kabla ya kuelekea katika kongamano hilo.