Saturday, November 25, 2023

JUKWAA LA WANAWAKE LALETA NEEMA KITUNDA

Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha akizungumza na wanawake wa Kata ya Kitunda jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo. Jukwaa hilo lilikuwepo hapo awali ila limefanyiwa uhuishwaji na wanawake wa kata hiyo.


Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Kitunda, Anna Haule (kulia) akizungumza wakati wa uzinduzi wa jukwaa hilo la kuwezesha wanawake kiuchumi ulifanyika jijini Dar es Salaam jana. Moja ya Lengo la Jukwaa hilo ni kuwa na sauti ya pamoja, kutafakari na kuibua miradi mbalimbali. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha, Diwani Viti Maalum, Eva Nyamoyo na Mwenyekiti wa UWT, Mwanaidi Makongo.]


Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha akikata keki kuashiria uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo.


Diwani Viti Maalum, Bi. Eva Nyamoyo akitoa somo la malezi ya watoto wakati wa uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo. Jukwaa hilo lilikuwepo hapo awali ila limefanyiwa uhuishwaji na wanawake wa kata hiyo.


Baadhi ya wanawake wa Kitunda wakihudhuria katika uzinduzi wa jukwaa hilo jijini jana.



Bibi Maendeleo Kata ya Kitunda, Betty Mzava akizungumza katika hafla hiyo.



Mtendaji Kata ya Kitunda, leticia Chipando, akitoa somo la usafi mahala pa kazi jijini Dar es Salaam jana wakati wa uzinduzi wa jukwaa la kuwezesha wanawake kiuchumi pamoja na kuzindua mfuko wa  malengo ya kuwa na kituo cha kulelea watoto waliokusudiwa na jukwaa hilo.

Mkurugenzi wa Merrymerry.tz, Mery Samson Chacha ( katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali wa Kitunda wakati baada ya kuzindua jukwaa hilo jijini Dar es Saaam jana.





                             

Saturday, November 18, 2023

WATEULE VICOBA WAKUTANA NA NEEMA YA OMTO

Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule akitoa elimu ya vicoba endelevu kwa wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho jijini Dar es Salaam jana. Mkurugenzi huyo alialikwa kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo.


Mwalimu wa Wateule Vicoba, Glory Munisi akitoa elimu kuhusu elimu ya fedha wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho kilichopo Ulongoni jijini Dar es Salaam jana. Wateule Vicoba inajumla ya vikundi 7 chini ya ,Mkurugenzi huyo.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo, Neema Mchau akizungumza wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni kuhusu masuala ya kuthamini familia pamoja na kuimarisa ndoa wakati wa hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho jijini Dar es Salaam jana.


Baadhi ya Wanachama wa Wateule Vicoba wakisikiliza kwa makini mada zinazotolewa katika maadhimisho hayo.


Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule (katikati), Katibu wa OMTO, Eliwaza Joseph na Mkurugenzi wa Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo, Neema Mchau wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza maadhimisho ya maika 12 ya Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni jijini Dar es Salaam jana. 

Mkurugenzi wa Taasisi ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization (OMTO), Anna Haule ( wa tatu kulia waliokaa ) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa serikali ya mtaa, walimu wa vicoba mbalimbali pamoja na wanachama wa Kikundi cha Vicoba cha Wateule kilichopo Ulongoni baada ya kumaliza hafla ya kuadhimisha miaka 12 ya kikundi hicho jijini Dar es Salaam jana. Mkurugenzi aliahidi kufanya mipango ya kuvisajili vikundi vyote 7 vilivyopo katika kikba hicho pamoja na kushirikiano nao ili kupata fursa zilizopo kwenye Vicoba endelevu kama CRDB Imbeju.