Friday, March 6, 2020

UMOJA WA WANAWAKE KITUNDA WAFANYA ZIARA KUTEMBELEA WENYE UHITAJI MAALUM

Afisa Maendeleo kata ya Kitunda, Sosina Soka ( wa pili kushoto ), Mkurugenzi wa Taasis ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization ( OMTO ), Anna Haule pamoja na Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda msaada wa taulo za wasichana kwa wasichana waliopo katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.

Baadhi ya Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakitoa msaada wa godoro, unga na sukari kwa Mmoja wa wakazi wa kata hiyo mwenye mazingira magumu kuelekea maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yatakayofanyika tarehe 8 machi. Umoja huo umefanya hafla ya kuwatembelea watu wenye uhitaji mbalimbali pamoja na kutembelea kituo cha watoto yatima cha Camp Caleb kilichopo mtaa wa Kipera kata ya Kitunda.  Matembezi hayo yamefanyika jijini Dar es Salaan jana.


Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakiongozana kwa pamoja wakiwa na misada yao kueleka kwa watu wenye uhitaji katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani. Ni miongoni wa mwa mila na desturi za umoja huo kusaidia wenye uhitaji maalum. Matembezi hayo yamefanyika jijini Dar es Salaan jana.

Baadhi ya Wanawake wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakisalimiana na Mmoja wa wakazi wa Kitunda, Bibi Tausi Ramadhani baada ya kuwasili mahali alipohifadhiwa kwaajili ya kumkabidhi msaada katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani. 

Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakikabidhi msaada wao kwa Bibi Tausi Ramadhani katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yanafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.


Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakikabidhi msaada wao kwa Mwakilishi wa Bibi anayeishi katika mazingira Magumu Bibi Salum  katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yanafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.

 Mwanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda akizungumza jambo na watoto yatima pamoja na wanaishi katika mazingira magumu baada ya kuwasili katika kituo cha Kulea watoto hao cha Camp Caleb kilichopo katika mtaa wa Kipera kata ya Kitunda kwa ajili ya kutoa msaada katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.

Baadhi ya Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakiimba nyimbo za kukataa unyanyasaji wa kijinsia baada ya kuwasili katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb kilichopo katika mtaa wa Kipera kata ya Kitunda kwa ajili ya kukabidhi msaada katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.

 Afisa Maendeleo kata ya Kitunda, Sosina Soka akigawa biskuti kwa  watoto wanaolelewa katika kituo hicho.

 Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wanaolelewa katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.

Afisa Maendeleo kata ya Kitunda, Sosina Soka ( wa pili kushoto ), Mkurugenzi wa Taasis ya Uwezeshaji Wajasiriamali ya Open Mind and Thoughts Organization ( OMTO ), pamoja na Wanachama wa Umoja wa Wanawake wa Kata ya Kitunda msaada wa chandarua kwa watoto waliopo katika kituo cha Kulea watoto yatima pamoja na wanaoishi katika mazingira magumu cha Camp Caleb katika kuelekea kilele cha Maadhimisho ya siku ya wanawake duniani ambayo kwa kata ya Kitunda yatafanyika tarehe 7 machi katika viwanja vya shule ya msingi Kerezange.

HABARI KATIKA PICHA














No comments:

Post a Comment